Machapisho

SOMO JIPYA

IJUE BIBLIA - Sehemu ya I

Picha
UTANGULIZI Biblia ni nini? Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 vilivyo andikwa na waandishi tofauti-tofauti 40 kwa takribani miaka 1500. Waandishi walikuwa wafalme, wavuvi, makuhani, viongozi wa serikali, wakulima, wachungaji, na madaktari. Biblia ni kitabu cha ajabu! Pamoja na kwamba vitabu vyake vimeandikwa na waandishi wengi tena kwa muda mrefu sana, bado kuna mtiririko na muunganiko wa ajabu kuanzia kitabu cha kwanza hadi cha mwisho. Hivyo basi kwa ujumla wake Biblia imeandikwa na wanadamu chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu wa Mungu

HIVI NDIVYO MTU ANAVYOOKOKA

Picha
Biblia husema ... “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka . Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa  hukiri hata kupata wokovu. ” [Warumi 10: 9,10] Ili mtu aokoke alizima...   1. Kuamini moyoni kuwa Mungu alimfufua Yesu katika wafu. Hii ina maana ya kuamini kazi nzima ya ukombozi wa mwanadamu ambayo Yesu Kristo aliikamilisha baada ya kufa msalabani na kufufuka siku ya tatu. Unapofika mahali pa kuyaangalia maisha yako na kuona kweli unamhitaji Yesu, basi hapo unapaswa kwanza kuamini kuwa Yesu alikufa msalabani kwa ajili yako ili upate msamaha wa dhambi. Biblia husema.....

MAANA YA WOKOVU

Picha
WOKOVU NI NINI? Kuokoka si lugha mpya masikioni kwako msomaji! Mara nyingi umesikia kwa watu mbalimbli na katika maeneo tofautitofauti kuwa mtu fulani “ amenusurika na janga la moto” au “ ameokolewa kwenye moto” au “jeshi la nchi fulani limekomboa mateka wake” au “ mtu amepona kwenye ajali mbaya”. Yote haya yanaelezea hali ya kunusurika au kuokoka kutoka kwenye hali hatarishi au kwenye mateso makali. Hii ndio hasa maana ya kuokoka Nini maana ya wokovu? Kuokoka ni kunusurika, kusalimika, kukombolewa, kufunguliwa au kupona kutoka katika janga au hatari fulani. Ili kuelewa hasa maana ya wokovu kibiblia, yakupasa kujua yafuatayo: