MAANA YA WOKOVU
WOKOVU NI NINI? Kuokoka si lugha mpya masikioni kwako msomaji! Mara nyingi umesikia kwa watu mbalimbli na katika maeneo tofautitofauti kuwa mtu fulani “ amenusurika na janga la moto” au “ ameokolewa kwenye moto” au “jeshi la nchi fulani limekomboa mateka wake” au “ mtu amepona kwenye ajali mbaya”. Yote haya yanaelezea hali ya kunusurika au kuokoka kutoka kwenye hali hatarishi au kwenye mateso makali. Hii ndio hasa maana ya kuokoka Nini maana ya wokovu? Kuokoka ni kunusurika, kusalimika, kukombolewa, kufunguliwa au kupona kutoka katika janga au hatari fulani. Ili kuelewa hasa maana ya wokovu kibiblia, yakupasa kujua yafuatayo: